Sauti ni mlio au tamko ambalo linatokana na kule kugusana kwa ala za kutamkia. Sauti huwakilishwa na alama //.

Kwa Mfano, /b/, /d/, /e/ n.k.

Lugha ya Kiswahili huwa na aina mbili kuu za sauti ambazo ni:

  • Konsonanti
  • Irabu
  • Silabi

Konsonanti

Sifa moja kuu ya konsonanti za Kiswahili ni kuwa; sauti hizi zinapotamkwa, hewa hubanwa/huzuiliwa kwenye ala za kutamkia. Kuna aina nyingi za konsonanti kutokana na ala zinazotumika katika kuzitamka na pia jinsi ya kuzitamka.

Konsonanti pia zinaweza ainishwa kutokana na sifa ya ghuna (h) na sighuna (gh). Kutokana na nyenzo hizi tatu, tunapata aina hizi za konsonanti:

Aina Za Konsonanti

Aina za sauti

*Sauti ghuna (h) ni zile konsonanti ambazo wakati zinapotamkwa, huwa kuna mtetemeko/mtikisiko wa nyuzi za sauti ilhali huwa hakuna mtetemeko wa nyuzi za sauti sauti sighuna (gh) zinapotamkwa.

Irabu

Pia zinajulikana kama vokali. Irabu za Kiswahili ni zile sauti ambazo zinapotamkwa, hewa huwa haizuiliwi/haibanwi kwenye ala za kutamkia.

Kuna aina tano za irabu za Kiswahili: /a/, /e/, /i/, /o/, /u/.

Irabu za Kiswahili huainishwa kwa kutumia vigezo viwili vikuu: sehemu ya ulimi na hali ya mdomo.

Kutokana na kigezo cha sehemu ya ulimi, tunapata irabu za mbele, kati na nyuma.

Sehemu ya Ulimi

sehemu ya ulimi

Hali ya Mdomo

Kutokana na kigezo hiki, tunapata irabu ambazo hutamkwa wakati midomo imetandazwa k.v /a/, /e/ na /i/.

Vilevile, kunazo irabu ambazo hutamkwa wakati midomo imevirigwa k.v /o/ na /u/.

SILABI

Silabi ni sauti mbili au zaidi zinazotamkwa kwa pamoja au kama sauti moja.

Silabi huwa hazina maana toshelezi. Kwa mfano; /b/ pamoja na /a/ zinaunda silabi ba.

Mifano katika neno: dak-ta-ri; shu-le; ma-ma; muk-ta-dha

Kuna aina mbili kuu za silabi za Kiswahili; silabi funge na silabi huru

Silabi funge/ambata

Hizi ni silabi ambazo huishia kwa konsonanti. Kwa mfano: Dak kwenye daktari; Kab kwenye kabla; Muk kwenye muktadha

Silabi huru/wazi

Silabi huru za Kiswahili ni zile silabi ambazo huishia kwa irabu. Maneno mengi ya Kiswahili huundwa kwa silabi huru.

Kwa mfano: mu kwenye mwa-li-mu; ma kwenye li-ma.