Vihisishi huwakilishwa kwa herufi I.

Ni aina za maneno ambazo huonyesha hisia. Kuna hisia mbalimbali zinazoonyeshwa na vihisishi.

kama vile:

  • Huzuni

    Kwa mfano: Salale!

  • Furaha

    Kwa mfano: Shabash! Oyee! Ahaa!

  • Mshangao

    Kwa mfano: Ala! Aka! Ebo! Masalale!

  • Kuakiki/Kukubali

    Kwa mfano: Hewaa! Naam!

  • Hisia za dharau

    Kama vile: Ebo! Po!

    Hisia ni nyingi. Vihisishi vinapotumiwa kwenye sentensi, alama ya kihisi (!) hutumiwa.