Vihusishi vya Kiswahili huwakilishwa na herufi H.

Ni aina ya maneno inayoonyesha uhusiano wa nomino na mazingira yake.

Mifano: Kando ya, mbele ya, kabla ya, katikati ya, katika n.k.

Mifano katika sentensi:

  • Mama alisimama katikati ya barabara.
  • Mtoto alicheza kando ya mto.
  • Mwanafunzi alifika kabla ya/mbele ya mwalimu.
  • Paka yuko chini ya meza.