Vitenzi huwakilishwa na herufi T.

Ni aina ya maneno ambayo huonyesha kitendo au hali katika sentensi.

Kwa mfano:

  • Mama anapika (kitendo)
  • Mwalimu ni mgonjwa (hali).

Zifuatazo ni aina mbalimbali za vitenzi vya Kiswahili:

Vitenzi halisi/Vikuu

Huonyesha kitendo halisi au kikuu au muhimu ambacho kinatendwa na mtendaji kwenye sentensi.

Kwa mfano:

  • Watoto wanacheza mpira.
  • Musa anasoma gazeti.

Vitenzi Visaidizi

Kinasaidiana na kitenzi kikuu ili kufafanua kitendo kikuu au kukifanya kueleweka zaidi.

kwa mfano:

Watoto walikuwa (kitenzi kisaidizi) wanacheza(kitenzi kikuu) mpira.

Vitenzi Vishirikishi

Ni aina za vitenzi ambazo hushirikisha vitu kihali, kitabia au kimazingira

Kwa mfano:

  • Maria ni msichana mkorofi; sisi tu wanafunzi wenye msimamo
  • Mama yangu si mkali.