Viwakilishi huwakilishwa na herufi W.

Ni aina za maneno ambazo hutumiwa kuwakilisha nomino; yaani viwakilisha hutumiwa badala ya nomino.

Kwa mfano, badala ya kusema: Yeye ni mtoto mtiifu. Yeye inawakilisha nomino katika sentensi hii.

Kuna aina nyingi za viwakilishi vya Kiswahili:

Viwakilishi vya Nafsi

Hutumika badala ya nomino zinazotaja nafsi; vinaweza kutokea kwa umoja au wingi.

Kwa mfano: Mimi- Sisi; Wewe-Nyinyi; Yeye- Wao

Viwakilishi Vionyeshi

Kwa mfano:

  • Hawa wanasumbua.
  • Wale wataimbia wageni.

Viwakilishi Viulizi

Kwa mfano:

  • Yupi ataimbia wageni?
  • Lipi lilioza?

Viwakilishi Vimilikishi

Kwa mfano: Lake lilipotea (Lake linaeza kuwa linawakilisha kitu chochote kinachopatikana katika ngeli ya LI-YA kama vile; tunda, gari).

Viwakilishi Virejeshi

Vinarejelea nomino; kama vile: Ambacho kilipotea; Kilichopotea; Ambaye alipotea; Aliyepotea.

Viwakilishi vya Sifa

Kwa mfano: Wazuri watatuzwa; Warefu wataajiriwa; Watiifu walitumiwa kama mfano.

Viwakilishi vya Idadi

Kama vile: Wawili walitumwa; Saba watasafiri kesho.

Idadi hizi za Kiswahili huwa hazichukui viambishi ngeli- sita, saba, tisa, kumi. Kwa hivyo, ni makosa kusema: wasita, wasaba, watisa, wakumi.

Viwakilishi vya Pekee

Hubainisha nomino inayotajwa.

Huchukua muundo wa –ote, o-ote, -enye, -enyewe na ingine.

Kwa mfano:

  • Yeyote atatumwa (ngeli za A-WA huwa yeyote kwa umoja).
  • Chochote kitatumika.
  • Mwenyewe atafua.
  • Mwenye gari atatumwa.
  • Kingine kilitupwa.

Viwakilishi vya A-Unganifu

Ni kama vile tu vivumishi vya sifa ila tu nomino hazitajwi kwenye viwakilishi.

Kwa mfano; Cha mama kilipotea; Ya wazee yaliibwa.